Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwendesha Mashtaka wa ICC awasiliana na viongozi wa kimataifa juu ya Darfur

Mwendesha Mashtaka wa ICC awasiliana na viongozi wa kimataifa juu ya Darfur

Luis Moreno Ocampo, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa juu ya Makosa ya Jinai ya Halaiki (ICC) yupo New York kwa madhumuni ya kuwasiliana na watendaji wa kimataifa – yaani UM na wawakilishi wa Afrika – kuhusu taratibu za kuwapatia raia wa Darfur hifadhi ziada na kukomesha vitendo vya uhalifu dhidi yao na kuhakikisha maamuzi na madaraka ya Mahakama juu ya suala hilo yanatekelezwa haraka kwenye eneo la mtafaruku la Sudan magharibi.