Baraza Kuu linazingatia pendekezo la kupiga vita ugaidi duniani
Baraza Kuu la UM limekutana wiki hii kwa siku mbili, kwenye kikao cha wawakilishi wote kuzingatia azimio la kupiga vita ugaidi duniani. Kulifanyika majadiliano maalumu yaliofanya mapitio juu ya lile azimio la 2006 la Kuratibu Mipango ya Pamoja Kupiga Vita Ugaidi Ulimwenguni.