Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Mpaka wa mwisho' wa uvuvi wahitajia usimamizi bora, FAO kuonya

'Mpaka wa mwisho' wa uvuvi wahitajia usimamizi bora, FAO kuonya

Baada ya miaka miwili ya mashaurianio na majadiliano, wiki hii wajumbe wanachama wa mataifa 191 wa Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) wamefanikiwa kuafikiana na kupitisha miongozo mipya ya kimataifa ili kudhibiti bora uvuvi, hasa ule uvuvi wa kina kikubwa baharini, ambapo mfumo wa ikolojia ni dhaifu na haraka kuharibika kama haujatunzwa kama inavyotakikana kisayansi.