Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uchumi wa 2008 duniani ni wa gizagiza, inasema UNCTAD

Uchumi wa 2008 duniani ni wa gizagiza, inasema UNCTAD

Shirika la UM juu ya Biashara na Maendeleo (UNCTAD) limetoa ripoti ya mwaka inayozingatia \'hali ya biashara na maendeleo kimataifa kwa 2008\'. Ripoti ilisema katika miaka ya karibuni nchi nyingi zinazoendelea zilionekana kufanikiwa kwenye maendeleo yao ya uchumi yenye kutia moyo.