Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usomali inahimizwa kurudisha amani wakati wa Ramadhan

Usomali inahimizwa kurudisha amani wakati wa Ramadhan

Mark Bowden, Mshauri Mkaazi wa UM juu ya Misaada ya Dharura kwa Usomali ametuma salamu maalumu, kwa niaba ya jamii ya UM, kutokea ofisi yao iliopo Nairobi, Kenya zilioukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na kuwatakia umma wa Usomali Ukarimu Mkuu kwa Ramadhan ya mwaka huu.