Hapa na Pale
Serge Brammertz Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama ya UM juu ya Makosa ya Vita kwa iliokuwa Yugoslavia (ICTR) amewasilisha ripoti maalumu kwa waandishi habari Ijumatatu (21 Julai) ya kupongeza kukamatwa kwa Radovan Karadzic, kiongozi wa kisiasa wa Waserb wa Bosnia na mtoro aliyekimbia adhabu ya sheria kwa muda mrefu katika Bosnia-Herzegovina. Karadzic alishikwa na wenye madaraka Serbia na sasa yupo kizuizini. Karadzic alishitakiwa rasmi na Mahakama ya ICTR miaka 13 iliopita kwa kuongoza makosa dhidi ya utu na mauaji ya halaiki kwa raia wa Bosnia-Herzegovina wasiokuwa Waserb - yaani Wacroat na WaIslamu wa huko. Tutakupatieni taarifa zaidi Ijumanne.