Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watumishi wa WHO wanajiandaa kurejea Iraq

Watumishi wa WHO wanajiandaa kurejea Iraq

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza wafanyakazi wa kimataifa walioondoshwa Iraq baada ya shambulio la Ofisi za UM za Baghdad katika Agosti 2003, wanajiandaa sasa hivi kurudi tena nchini humo kutekeleza majukumu yao. WHO imesisitiza hatua hii itaisaidia Iraq kukabiliana vizuri zaidi na matatizo ya kiutu yaliojiri nchini, na vile vile itaipatia marekibisho yanayohitajika kuimarisha vizuri zaidi sekta ya afya ya jamii, hasa kwenye mazingira magumu ambayo yametanda Iraq kwa sasa. ~~