Usalama wa wapinzani Zimbabwe wazingatiwa na IPU
Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mabunge ya Kimataifa (IPU) ambayo inakutana Geneva imeripoti kuingiwa wasiwasi kwamba bunge la Zimbabwe halijakutana kwa zaidi ya miezi mitatu, kufuatia uchaguzi wa tarehe 29 Machi (2008).