Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WIPO imeripoti kuongezeka duniani kwa maombi ya hakimiliki

WIPO imeripoti kuongezeka duniani kwa maombi ya hakimiliki

Shirika la UM juu Ya Hakimiliki za Taaluma Duniani (WIPO) kwenye Ripoti ya 2008 kuhusu maombi ya umiliki wa uvumbuzi wa vitu vunavyotengenezwa, kuuzwa na kutumiwa na umma wa kimataifa, imebanisha kwamba kumepatikana muongezeko mkubwa wa maombi hayo, katika miaka ya karibuni, hasa kutokea mataifa ya Uchina, Jamhuri ya Korea (Korea ya Kusini) na Marekani ambapo wavumbuzi wa mambo kadha wa kadha, na vitu mbalimbali, walitaka wapatiwe hati ya hakimiliki juu ya uvumbuzi wao.