UNHCR imesafirisha Kenya misaada ziada ya kiutu
Mnamo mwisho wa wiki iliopita, Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) lilipeleka nchini Kenya mahema 2,345 yatakayotumiwa na makumi elfu ya zile familia zilizong’olewa makwao baada ya machafuko kufumka nchini mwanzo wa mwaka kufuatia uchaguzi.