Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM wasaidia kuwapatia watoto wa Cameroon chanjo kinga

UM wasaidia kuwapatia watoto wa Cameroon chanjo kinga

UM ikishirikiana na Serikali ya Cameroon pamoja na zile jumuiya zisio za kiserekali zimefanikiwa kukamilisha huduma ya kuwachanja watoto 35,000 dhidi ya shurua na maradhi ya kupooza/polio katika wilaya ya Koussei, kaskazini-mashariki ya Cameroon. Asilimia kubwa ya watoto hawa walikuwa ni raia wa Chad waliohamia Cameroon baada ya machafuko kufumka kwenye mji mkuu wa N’Djamena, Chad.