Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usalama wa raia Darfur Magharibi unatia kiherehere

Usalama wa raia Darfur Magharibi unatia kiherehere

Ijumapili Mshauri wa UM juu ya Misaada ya Kiutu katika Sudan, Ameerah Haq pamoja na Rodolphe Adada, Mjumbe Maalumu wa Ubia wa UM/UA na pia Mkuu wa Vikosi Mseto kwa Darfur (UNAMID) walitoa risala iliobainisha kuingiwa na ‘khofu kuu’ juu ya usalama wa maelfu ya raia wanaoishi katika sehemu ya Jebel Muun, Darfur Magharibi kutokana na hujuma za karibuni kwenye maeneo yao.