Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

OHCHR inalaani ukiukaji wa haki za binadamu Chad

OHCHR inalaani ukiukaji wa haki za binadamu Chad

Ofisi ya Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki Binadamu (OHCHR) imearifu kupokea taarifa za kutia wasiwasi zilizoonyesha vikosi vya usalama vya Serikali viliwateka nyara viongozi kadha wa upinzani, pamoja na kuwashika viongozi wa jumuiya za kiraia na kuwatia kizuizini baada ya kutukia mashambulio ya waasi karibuni kwenye mji mkuu wa N’Djamena, Chad .