Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

'Jukumu la polisi katika kutunza amani ni lazima litambuliwe': asema Mkuu wa Polisi wa UNMIS

Kai Vittrup, Kamishna wa Polisi wa Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani Sudan (UNMIS) ameliambia Shirika la Habari la UM kwamba Mataifa yote Wanachama ya UM yanawajibika kutambua jukumu muhimu la kazi za polisi wa kimataifa katika uendeshaji wa operesheni za amani za UM. Kamishna Vittrup aliyahimiza Mataifa Wanachama yaridhie pendekezo la kupeleka raia polisi wa vyeo vya juu, katika Darfur kusaidia operesheni zijazo za ulinzi wa amani za UM.

Masaibu ya wahamaji wa Pembe ya Afrika yaomba suluhu ya kimataifa

Shirika la Kimataifa juu ya Wahamaji (IOM) limeripoti kuwa linahitajia kufadhiliwa msaada wa dharura najamii ya kimataifa, utakaoliwezesha kununua vifaa vya kusajili na kuhifadhi takwimu za wale wahamaji na watu wenye kuomba hifadhi ya kisiasa kutoka eneo la Pembe ya Afrika, ambao wameanza kuwasili kwa wingi katika Yemen hivi karibuni baada ya kuvuka Ghuba ya Aden.

Hapa na pale

Tarehe 10 Septemba iliadhimishwa na UM kuwa ni ‘Siku ya Kuzuia Vitendo Karaha vya Kujiua Duniani’, hasa ilivyokuwa takwimu za wataalamu wa kimataifa zimethibitisha kuwa katika kila nukta 30 mtu mmoja huwa anajiua ulimwenguni kwa sababu kadha wa kadha.

Ziara ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Sudan

KM wa UM Ban Ki-moon wiki hii alifanya ziara ya siku nne nchini Sudan, ikiwa miongoni mwa juhudi za kimataifa, kuleta hatima ya mgogoro na vurugu liliolivaa jimbo la magharibi la Darfur. Kadhalika, KM alichukua fursa ya kujionea binafsi aina ya mazingira yatakayovikabili vikosi mseto vya UM na Umoja wa Afrika wa AU vitkavyopelekwa Darfur mwakani.~