Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Jukumu la polisi katika kutunza amani ni lazima litambuliwe': asema Mkuu wa Polisi wa UNMIS

'Jukumu la polisi katika kutunza amani ni lazima litambuliwe': asema Mkuu wa Polisi wa UNMIS

Kai Vittrup, Kamishna wa Polisi wa Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani Sudan (UNMIS) ameliambia Shirika la Habari la UM kwamba Mataifa yote Wanachama ya UM yanawajibika kutambua jukumu muhimu la kazi za polisi wa kimataifa katika uendeshaji wa operesheni za amani za UM. Kamishna Vittrup aliyahimiza Mataifa Wanachama yaridhie pendekezo la kupeleka raia polisi wa vyeo vya juu, katika Darfur kusaidia operesheni zijazo za ulinzi wa amani za UM.