Janga la njaa lanyemelea Sudan Kusini WFP yatiwa hofu kubwa
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP linashtushwa na hofu mpya ya viwango vya janga la njaa wakati huu likikabiliwa na ukata wa fedha za msaada huko Sudani Kusini
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP linashtushwa na hofu mpya ya viwango vya janga la njaa wakati huu likikabiliwa na ukata wa fedha za msaada huko Sudani Kusini
Karibu watoto milioni 5 watahitaji msaada wa kibinadamu mwaka huu Sahel ya Kati kutokana na machafuko yanayoendelea limeonya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF likisema idadoi hiyo ni ongezeko kubwa kutoka milioni 4.3.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameikumbusha dunia kwamba mauaji ya maangamizi makuu au Holocaust ni uhalifu mbaya zaidi kuwahi kutokea duniani na tunapowakumbuka waathirika ni jukumu la dunia kuhakikisha kwamba uhalifu huu asilani haurejei tena
Serikali ya Myanmar leo imeamriwa na mahakama ya haki ya Umoja wa Mataifa ICJ, kuzuia machafuko yanayoweza kusababisha mauaji ya kimbari kwa watu wa kabila la Rohingya ambao ni Waislam wachache na kulinda ushahidi wowote wa uhalifu wa siku za nyuma dhidi ya watu hao.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ameungana na dunia kuukaribisha mwaka mpya wa 2020 akiisihi dunia kudumisha amani hasa muongo wa utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu au SDGs ukianza.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amempongeza kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis kwa kupunguza madhila kwa watu na kutetea hadhi ya haki za binadamu.
Nchini Ujerumani mafunzo mahsusi yanayotolewa na kampuni za kijerumani kwa wakimbizi yameleta siyo tu matumaini kwa wakimbizi bali pia kusaidia kujenga utangamano na jamii zinazowazunguka.
Watu zaidi ya milioni 168 kote duniani mwaka 2020 watahitaji msaada wa kibinadamu na ulinzi katika migogoro inayoendelea kwenye nchi Zaidi ya 50 limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu mimasuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA.
Kuelekea siku ya UKIMWI duniani tarehe Mosi mwezi ujao wa Desemba, Doreen Moraa Moracha, msichana kutoka Kenya ambaye anaishi na virusi vya UKIMWI amekuwa changamoto kubwa katika kumaliza unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi au VVU.
Umoja wa Mataifa umesema jamii ikiwa ni pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali, asasi za kiraia na wanaharakati wana mchango mkubwa katika vita dhidi ya UKIMWI.