UNMISS wakarabati mahakama na kujenga jela mpya jimboni Equatorial magharibi
Katika kuhakikisha wanawavutia wakimbizi wa ndani kurejea makwao, ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS, umekarabati na kukabidhi jengo la mahakama pamoja na kujenga jengo jipya la jela huko jimboni Equatorial Magharibi katika kaunti ya Maridi.