Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Mwanamke kijana wa Kiukreni akitembea katikati ya magofu ya nyumba ya babu yake huko Irpin.
© UNICEF/Diego Ibarra Sánchez

UN na wadau waomba dola bilioni 5.6 kusaidia mamilioni walioathirika na vita Ukraine

Wakati vita nchini Ukraine ikikaribia kuingia mwaka wa pili, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR leo kwa pamoja wameomba jumla ya dola bilioni 5.6 ili kupunguza madhila yanayowakabili mamilioni ya watu walioathirika na vita nchini Ukraine.

Sauti
2'19"
Laila Baker Mkurugenzi wa UNFPA wa nchi za Kiarabu, atembelea Aleppo, Syria kufuatia tetemeko kubwa la ardhi
UNFPA

UNFPA: Tetemeko la ardhi limevunja si tu majengo ya Syria bali pia matumaini yao

Mkuu wa kanda ya nchi za kiarabu katika shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu duniani, na afya ya uzazi, UNFP Laila Baker amesema pamoja na shirika hilo kuhitaji fedha ili kuweza kuwahudumia wanawake na wasichana waliathiriwa na matetemeko nchini Turkiye na Syria lakini kila sehemu anapopita nchini Syria wanawake hutoa ombi moja tu nalo ni kuhitaji amani.

Sauti
4'24"
Mwandishi wa habari akitangaza katika Radio Miraya nchini Sudan Kusini.
UNMISS/Isaac Billy

Radio na nafasi yake ya ujenzi wa amani

Hii leo ni siku ya redio duniani ambapo Umoja wa Mataifa unamulika nafasi ya chombo hicho kilichobuniwa takribani karne moja iliyopita katika kukuza na kujenga amani  wakati huu ambapo pia ni miaka 75 tangu kuanzishwa kwa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.

Sauti
1'44"
Chakula kinasambazwa kwa watu waliokimbia makazi yao baada ya tetemeko la ardhi huko Aleppo, Syria.
© Al-Ihsan Charity

Tunataka kuwafikia waathirika wote japo kuna kikwazo cha usalama katika baadhi ya maeneo - WFP Syria

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kupeleka na kusambaza misaada nchini Uturuki na Syria ili kusaidia walioathiriwa na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyotokea Jumatatu wiki hii na kujeruhi, kuua maelfu na kuharibu miundombinu. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) lina lengo la kuwafikia watu nusu milioni katika nchi zote mbili ijapokuwa kuna changamoto za kiusalama katika baadhi ya maeneo.

Sauti
2'59"