Dola bilioni 4.3 zahitajika kwa ajili ya mahitaji ya kibinadamu Yemen 2023:UN
Wahisani wa kimataifa wanakutana leo mjini Geneva Uswis kwa ajili kutanabaisha kuhusu zahma ya kibinadamu inayoendelea nchini Yemen na kuchangisha fedha za kufadhili operesheni za kibinadamu nchini humo. Mkutano huo wa ngazi ya juu wa kuchangisha fedha kwa ajili ya Yemen umeandaliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na serikali za Sweden na Uswis.