Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Familia ikiwa imekaa kwenye makazi ya wakimbizi wa ndani mjini Aden Yemen
© UNHCR/Ahmed Al-Mayadeen

Dola bilioni 4.3 zahitajika kwa ajili ya mahitaji ya kibinadamu Yemen 2023:UN

Wahisani wa kimataifa wanakutana leo mjini Geneva Uswis kwa ajili kutanabaisha kuhusu zahma ya kibinadamu inayoendelea nchini Yemen na kuchangisha fedha za kufadhili operesheni za kibinadamu nchini humo. Mkutano huo wa ngazi ya juu wa kuchangisha fedha kwa ajili ya Yemen umeandaliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na serikali za Sweden na Uswis. 

Sauti
2'40"
Jengo lililoharibiwa katikati mwa Kharkiv, Ukraine.
© UNOCHA/Matteo Minasi

Viongozi watoa maoni yao baada ya uamuzi wa Baraza Kuu la UN dhidi ya Urusi

Vita ya Ukraine ikiwa inaingia mwaka wake wa pili, wawakilishi mbalimbali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wametoa maoni yao kufuatia uamuzi kwa njia ya kura uliofanywa na Kikao Maalumu cha  dharura cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio jipya la kutaka amani ya haki na ya kudumu nchini Ukraine na kwamba Urusi bila masharti yoyote iondoe mara moja majeshi yake katika ardhi ya Ukraine. 

Sauti
2'22"
Mkoani Njombe kusini mwa Tanzania, mapishi mbalimbali kutokana na matumizi ya mikunde. Hii inafuatia mafunzo yaliyowezeshwa na FAO na AgriConnect.
FAO Tanzania

Nyama ikiingia mezani, mikunde hunyanyapaliwa- FAO

Jamii ya mikunde! Wengi wanaitambua zaidi kama ni kunde zenyewe, na maharagwe lakini ni zaidi ya hiyo. Kuna choroko, mbaazi, dengu, njegere na kadha wa kadha ambapo kutokana na umuhimu wake sio tu kiuchumi bali pia katika lishe ya binadamu, kurutubisha udongo na pia kuhimili mabadiliko ya tabianchi, ndio maana Umoja wa Mataifa unapigia chepuo.

Sauti
4'55"
Mkulima akimwagilia mboga kwa kutumia maji kutoka bwawa la Guerin-Kouka  nchini Togo
FAO

Nchi za Afrika wekeni mikakati ya usimamizi bora wa matumizi ya maji- FAO

Ni wakati kufikiria upya jinsi ya kutumia maji kwa njia endelevu na yenye uwiano huku ubunifu katika kilimo ukiwa kitovu cha mipango yote,  amesema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limesema  Qu Dongyu hii leo wakati akizungumza na viongozi na wataalamu wa Afrika kwenye warsha ya kwanza ya kikanda kuhusu mwelekeo wa matumizi ya maji barani Afrika, warsha inayofanyika nchini Zimbabwe.

Sauti
1'47"
Ndoto ya Thérèse (pichani) ni kuwa Gavana wa jimbo la Tanganyika. Hapa ni katika darasa jipya lililojengwa kwenye shule ya msingi ya Lubile jimboni Tanganyika kwa msaada wa UNICEF na Education Cannot Wait.
© UNICEF/Josue Mulala

UNICEF na ECW yarejesha matumaini kwa watoto waiotumikishwa vitani DRC

Mradi mpya wa shule  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC uliozinduliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF na wadau wake kwa ufadhili kutoka mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kuchagiza elimu kwenye maeneo ya mizozo, Education Cannot Wait, ECW, au Elimu Haiwezi Kusubiri umewezesha watoto waliokuwa wametumikishwa vitani kuanza kurejea kwenye masomo na hata kutangamana na wenzao kwa amani.  

Sauti
2'45"
Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanasafirisha misaada kibinadamu kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi kutoka Türkiye kwenda kaskazini magharibi mwa Syria.
© UNOCHA/Madevi Sun Suon

Ujumbe wa mashirika ya Umoja wa Mataifa watembelea walioathirika na tetemeko nchini Syria

Ujumbe wa mashirika saba ya Umoja wa Mataifa umetembelea hospitali na kliniki zinazoungwa mkono na shirika lisilo la kiserikali la Misaada na Maendeleo la Syria au SRD, Kaskazini Magharibi mwa Syria na kujionea athari za tetemeko la Ardhi lililoikumba nchi hiyo wiki mbili zilizopita pamoja na kujionea usambazaji wa misaada iliyotolewa na Umoja wa Mataifa.

Sauti
2'28"
Msaidizi wa Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Suluhisho la Wakimbizi wa Ndani Robert Piper akizungumza na mkazi wa makazi ya Barwaqo IDP huko Baidoa, Somalia tarehe 13 Februari 2023.
UN Photo / Ali Bakka

Ziara yangu ya kwanza Somalia ni somo - Robert Piper

Robert Piper akiwaeleza kwa ufupi wawakilishi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa kimataifa kuhusu nia ya ziara yake anasema, “nimekuja kuwasikiliza Wakimbizi wa Ndani na kuelewa hali zao na kujifunza kutoka kwa familia ya Umoja wa Mataifa na wadau wetu kuhusu jinsi tunavyokuungeni mkono katika changamoto hii.”  

 

Sauti
3'35"