Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Vipimo vya virusi vya ukimwi.
Public Health Alliance/Ukraine

Vipimo vya VVU vyapungua UNITAID waomba ufadhili zaidi

Kuelekea kilele cha siku ya UKIMWI Duniani Desemba 1, Shirika la Umoja wa Mataifa la kufanikisha upatikanaji wa dawa za tiba kwa gharama nafuu, UNITAID limesema usumbufu na ucheleweshaji wa huduma za VVU unaosababishwa na janga la COVID-19 ulisababisha kupungua kwa vifaa vya upimaji na utambuzi wa VVU kwa kiwango kikubwa ambacho hakijawahi kuonekana ndani ya miongo miwili.

Sauti
2'28"
Taswira kutoka juu ya mafuriko katika kambi ya wakimbizi ya Alganaa kwenye jimbo la White Nile nchini Sudan.
UNHCR Video

Hatujawahi kuona mafuriko kama  haya Sudan- Mkazi White Nile

Tumeishi hapa tangu miaka ya 1950 na katu hatujawahi kushuhudia mafuriko kama haya, amesema mkazi wa jimbo la White Nile nchini Sudan ambako mafuriko makubwa yamesababisha wakimbizi wa ndani kusaka hifadhi kwa wenyeji wao huku shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wadau wakiendelea kusambaza misaada ya kibinadamu. John Kibego na maelezo zaidi.

 

Sauti
2'2"