Vijana tusidhalilishane mitandaoni bali tuelimishane-Ogola
Mitandao ya kijamii ina hatari na athri kubwa zaidi kwa vijana inapotumiwa vibaya amesema balozi mwema wa wakfu wa Umoja wa Mataifa au UN Foundation Philip Ogola.
Mitandao ya kijamii ina hatari na athri kubwa zaidi kwa vijana inapotumiwa vibaya amesema balozi mwema wa wakfu wa Umoja wa Mataifa au UN Foundation Philip Ogola.
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Yemen, Martin Griffiths, amekaribisha hatua ya kundi la Ansar Allah nchini humo ya kuwaachilia huru wafungwa.
Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ameiambia Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa anakusudia baadaye hii leo kuuleza mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 pamoja na mambo mengine, kuhusu hatua za maendeleo ambazo Burundi imepiga na pia kuiomba jumuiya ya kimataifa kuiunga mkono nchi yake.
Maandalizi ya mwishomwisho yanaendelea kwenye kituo cha muda cha Gashora nchini Rwanda ambako kundi la kwanza la wakimbizi na waomba hifadhi lilitarajiwa kuwasiku juma hili.
Mjadala Mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74, ukiingia siku ya nne hii leo kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani, Tanzania imesema imetenga asilimia 32 ya eneo la nchi kama hifadhi ya misitu kama njia mojawapo ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Katibu Mkuu wa kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD Dkt. Mukhisa Kituyi amesema teknolojia ya kuwa na fedha kwenye mtandao wa simu hadi mashinani itakuwa na maana zaidi pale watu watatumia fedha hizo kujiongezea kipato.
Jukwaa la kimataifa la vyuo vikuu barani Afrika na ughaibuni kuhusu malengo ya maendeleo endelevu na mustakabali wa elimu katika bara hilo, limezinduliwa rasmi kwenye makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani.
Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya usafirishaji majini, wito umetolewa kuongeza idadi ya wanawake katika tasnia hiyo.
Tumefika hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuungana na nchi wanachama kuelezea ambayo Kenya imeyafanya katika kuhakikisha inaendana na vipaumbele vya mkutano huu wa Baraza Kuu la Umoja huo UNGA74 ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ujumuishwaji na ushirikiano wa kuhakisha utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs ifikapo mwaka 2030.
Tangu kupitishwa kwa mkataba wa haki za mtoto miaka 30 iliyopita pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana kote duniani bado vita imesalia kuwa chanzo kubwa ya ukiukwaji wa haki za mtoto na bado kuna nchi hazijaridhia mkataba huo amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.