Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, (kulia) akiwa na Waziri wa Mambo ya nje wa Burundi  Ezéchiel Nibigira  baada ya mazungumzo yao jijini New York, Marekani
Picha ya UN /Eskinder Debebe

Burundi twafanya uchaguzi mwakani, tuungeni mkono- Waziri Nibigira

Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ameiambia Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa anakusudia baadaye hii leo kuuleza mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 pamoja na mambo mengine, kuhusu hatua za maendeleo ambazo Burundi imepiga na pia kuiomba jumuiya ya kimataifa kuiunga mkono nchi yake.

Sauti
2'12"
Wenyeji wa Watamu, Kenya washirikiana na mamlaka kuondoa taka ya plastiki kutoka kwenye ufukwe wa bahari.
Cyril Villemain/UNEP

Elimu, ujumuishwaji na mabadiliko ya tabianchi ni baadhi vya vipaumbele vya Kenya:rais Kenyatta

Tumefika hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuungana na nchi wanachama kuelezea ambayo Kenya imeyafanya katika kuhakikisha inaendana na vipaumbele vya mkutano huu wa Baraza Kuu la Umoja huo UNGA74 ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ujumuishwaji na ushirikiano wa kuhakisha utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs ifikapo mwaka 2030.

Sauti
2'4"