Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ushirikiano baina ya vyuo vikuu utasaidia kuinua elimu Afrika- Profesa Miyamueni

Mabango ya maendeleo endelevu kama yanavyoonekana katika viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani Septemba 20,2019
UN News/Conor Lennon
Mabango ya maendeleo endelevu kama yanavyoonekana katika viwanja vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani Septemba 20,2019

Ushirikiano baina ya vyuo vikuu utasaidia kuinua elimu Afrika- Profesa Miyamueni

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Jukwaa la  kimataifa la  vyuo vikuu barani Afrika na ughaibuni  kuhusu malengo ya maendeleo endelevu na mustakabali wa elimu  katika bara hilo, limezinduliwa rasmi kwenye makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York  Marekani.  

Akizungumza na UN News Idhaa ya Kiswahili kandoni mwa mkutano huo, Profesa Antoine Kiamiantako Miyamueni, mdadhiri wa masuala ya uchumi katika chuo kikuu cha Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ( DRC)  amesema mkutano huo ni muhimu katika maendeleo ya elimu ya vyuo vikuu nchini DRC na barani Afrika kwa kuwa unajikita na changamoto zinazokabili bara la Afrika katika sekta ya elimu.

(Sauti ya Profesa Miyamueni)

Nchini zetu na vyuo vyetu vinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa utaalamu. Tunatarajia kwamba  katika mkutano huu tutaweza kutengeneza ushirikiano baina ya vyuo vyetu pamoja na vyuo vikuu vya nchi zilizoendelea  kaskazini .

Na kuhusu changamoto zinazokabili sekta ya elimu DRC amesma

(Sauti ya Profesa Miyamueni)

Elimu nchini kwetu iko katika viwango duni  sana kwasababu walimu hawafundishi ipasavyo kwa ukosefu wa   mishahara na motisha. Matokeo yake ni kwamba wanafunzi wanaojiunga na chuo kikuu wanakosa elimu bora.

Profesa Miyamueni ameota wito wa mshikamano wa nchi za Kiafrika katika sekta ya elimu ili kuboresha mustakabali wa elimu kwa ajili ya vizazi vijavyo.