Serikali na upinzani wanaposhikamana hakuna linaloharibika
Azma ya serikali ya Colombia na kikundi cha FARC ya kuhakikisha wanatekeleza makubaliano ya amani, imekuwa ni chachu ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa.
Azma ya serikali ya Colombia na kikundi cha FARC ya kuhakikisha wanatekeleza makubaliano ya amani, imekuwa ni chachu ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa.
Maeneo mapya 13 ya urithi wa kilimo yametajwa na shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na kutambuliwa rasmi kama mifumo ya urithi wa kilimo muhimu duniani-GIAHS.
Jamii ya asili wanahaha kila uchao kuhakikisha kwamba wanapata haki yao ya msingi hususan ile ya ardhi. Jamii hii hukumbwa na misukosuko mingi hasa inapodai haki ya ardhi yao ya asili ambayo ina maana kubwa kwao kuliko inavyofikiriwa.
Uchumi wa nchi za Afrika zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara unatabiriwa kukua kwa asilimia 3.1 mwaka huu wa 2018 na kwa asilimia 3.6 mwaka 2019.
Zaidi ya watoto 200 wameachiliwa huru na makundi yenye silaha nchini Sudan Kusini na idadi hiyo imefanya watoto walioachiliwa huru na makundi hayo tangu mwanzo wa mwaka huu 2018 ifikie 500.
Awali wananchi walipata shida kufika polisi ili kueleza madhila yao, lakini hivi sasa Umoja wa Mataifa umeweka mazingira ambamo kwayo wananchi wanaripoti polisi madhila yanayowakumba kwa urahisi na pia bila gharama yoyote.
Uchumi wa dunia unazidi kupanda taratibu licha ya matatizo ya hapa na pale, imesema ripoti mpya ya shirika la fedha duniani la IMF inayochunguza mwelekeo wa uchumi wa dunia
Baada ya ziara ya siku sita nchini Myanmar, Afisa mwandamizi wa Umoja wa Mataifa anaona kabisa ya kwamba wakimbizi wa Rohingya walioko Bangladesh bado wana hofu kubwa ya kurejea nyumbani ingawa jitihada za mazungumzo zinaendelea ili warejee Myanmar.
Kuwasikiliza na kuwashirikisha Wayemen katika mgogoro unaowahusu ni jambo la muhimu sana kwani suluhu ya vita nchini Yemen inaweza kutoka miongoni mwao na hasa kwa viongozi wao kuweka tofauti zao kando na kuafikiana sio kwa njia ya vita bali kupitia majadiliano.
Umoja wa Mataifa unahimiza kuleta maendeleo kupitia malengo yake ya maendeleo endelevu SDGs.Mathalani lengo namba moja la kutokomeza umaskini kwa ifikapo mwaka wa 2030. Kwa mantiki hiyo wanawake wa wilaya ya Lwengo, Kusini mwa Uganda nao wameamua kujifunga kibwebwe kuweza kutokomeza umaskini . Wameanzisha soko lao ambalo linauza bidhaa mbalimbali za matunda kama vile nyanya , na mboga za majani. Siraj Kalyango amevinjari eneo hilo na kuzungumza na baadhi ya wanawake hao na kutuandalia Makala ifuatayo.