Mabadiliko ya tabianchi yaleta zahma kwa mamilioni 2017:UN
Mwaka wa 2017 umeelezwa kama ulioshudia matukio yaliyofurutu ada ya hali ya hewa na hivyo kuwafanya mamilioni ya watu duniani kuteseka. Hivyo Umoja wa Mataifa unasema si hadhithi tena bali athari za mabadiliko ya tabia nchi zimeanza kushudiwa hususan katika jamii zilizo hatarini zaidi.