Ajira kwa vijana duniani inasuasua; hali ngumu zaidi kwa vijana wa kike- ILO
Suala la vijana kupata ajira tena kujikwamua kutoka hali ngumu ya maisha baada ya janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 limeendelea kusuasua, imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO iliyotolewa leo kuelekea siku ya vijana hapo kesho, ambapo shirika hilo linasema hali hiyo inathibitisha kuwa COVID-19 iliathiri zaidi vijana kuliko marika mengine, vijana wa kike wakiathirika zaidi.