Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Viki Bokanda, ingawa ni mvulana mwenye umri wa miaka 15 anajifunza  ushoni kwenye kituo cha mafunzo stadi kwa wasichana  huko Kisangani, Kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
© UNICEF/UN0507530/Frank Dejongh

Ajira kwa vijana duniani inasuasua; hali ngumu zaidi kwa vijana wa kike- ILO

Suala la vijana kupata ajira tena kujikwamua kutoka hali ngumu ya maisha baada ya janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 limeendelea kusuasua, imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO iliyotolewa leo kuelekea siku ya vijana hapo kesho, ambapo shirika hilo linasema hali hiyo inathibitisha kuwa COVID-19 iliathiri zaidi vijana kuliko marika mengine, vijana wa kike wakiathirika zaidi.

 

Mtoto Alex akiw akwenye mashine ya kumsaidia kupata hewa ya oksijeni katika kituo cha watoto wachanga, Ukraine.
Vayu Global Health/Unitaid

Mashine za kusaidia watoto kupumua zapelekwa Ukraine; ni ubunifu kutoka Kenya

Mashine 220 za kusaidia watoto wachanga kupata hewa ya oksijeni kutokana na kuwa hatarini kufariki dunia baada ya kuzaliwa ambazo zimetengenezwa nchini Kenya kwa msaada wa shirika la Umoja wa MAtaifa la kufanikisha upatikanaji wa dawa na tiba kwa gharama nafuu UNITAID zimepelekwa nchini Ukraine wakati huu ambapo vita vinakwamisha huduma za uzazi na kujifungua. 

Sauti
2'3"