Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wasichana katika shule ya Jean Vcolmomb huko Bangui, Jamhuri ya Afrika ya Kati.
©Education Cannot Wait

Mradi wa "Elimu haiwezi kusubiri" waonesha mafanikio makubwa katika kuwapatia elimu wasichana na wavulana walio katika maeneo ya mizozo

Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Elimu Haiwezi kusubiri Education Cannot Wait (ECW), ambao ni mfuko wa kimataifa wa elimu katika maeneo ya dharura na migogoro ya muda mrefu, umetoa Ripoti yake ya Mwaka ya Matokeo, ambayo imefichua kuwa licha ya msukosuko wa kimataifa, mfuko huo na washirika wake wameendelea kupanua wigo wao wa utoaji msaada. 

Familia za waliokimbia makaiz yao sababu ya machafuko wakiwa wamepata hifadhi huko Tambura nchini Sudan Kusini
UNMISS

Nitarina asali na kuuza dumu moja dola 50- Mnufaika wa mafunzo Sudan Kusini

Nchini Sudan Kusini, zaidi ya wakimbizi 50 waliorejea nyumbani pamoja na wakimbizi wa ndani eneo la Tambura jimboni Equatoria Magharibi wamenufaika na mafunzo ya stadi za kuwawezesha kupata kipato, mafunzo yaliyotolewa kwa pamoja na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani Sudan Kusini ,UNMISS na shirika la kiraia la wanawake, ANIKA. Tupate maelezo kamili kutoka kwa Assumpta Massoi. 

Sauti
2'30"
Kundi la watu wakikataana na chuki na ubaguzi unaotegemea kabila na dini katika Jamhuri ya Afrika ya Kati. (2017)
OCHA/Yaye Nabo Sène

Viongozi wa serikali na dini lindeni waathirika wa ukatili wa dini: Guterres

Hii leo dunia ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya kuwakumbuka waathirika wa vitendo vya ukatili kutokana na dini na imani zao ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema siku hii ni maalum kwa ajili ya kutoa heshima kwa wale ambao wamepoteza maisha au ambao wameteseka kwa sababu ya kutafuta haki zao za kimsingi za uhuru wa mawazo, dhamiri, na dini au imani.