Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto akiwa amesimama karibu na pampu ya maji iliyozingirwa na maji ya mafuriko huko Gatumba nchini Burundi.
© UNICEF/Karel Prinsloo

UNICEF imetuepusha na maji yenye wadudu- Wakazi wa Cibitoke

Tukiwa tunaelekea ukingoni mwa wiki ya maji duniani , nchini Burundi mradi uliotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa msaada wa serikali ya Japan umesaidia wakazi wa eneo la Cibitoke nchini Cibitoke siyo tu kuondokana na unywaji wa maji machafu  yenye wadudu, bali pia kuepusha watoto dhidi ya magonjwa na watoto wa shule kuondokana na zahma ya kutembea muda mrefu kwenda kuteka maji badala ya kwenda shuleni.

Taa za sola zinazotumiwa na wavuvi katika Ziwa Victoria Tanzania
UN NEWS/ Evarist Mapesa

Mwanza Tanzania wavuvi wazipa kisogo karabai na kugeukia taa za sola ili kujilinda wao na mazingira

Mwaka huu wa 2022 ulitangazwa na Umoja wa Mataifa kuwa mwaka wa uvuvi wa kiwango kidogo ukilenga wavuvi wanaotumia teknolojia za kiwango cha chini, sababu ni kuwamulika na kufahamu changamoto zao na kisha kuwajengea uwezo ili uvuvi wao uwe endelevu, usioharibu mazingira na wakati huo huo wajipatie kipato. Nchini Tanzania tayari hilo linafanyika kwa ushirikiano na wadau.

Leo ni Siku ya uhuru wa Ukraine hapa ni mjini Kyiv
© UNDP Ukraine/Krepkih Andrey

Miezi sita ya vita nchini Ukraine haya ni baadhi ya yaliyofanywa na WFP

Hii leo imetimia miezi sita rasmi tangu kuanza kwa vita baina ya Ukraine na Urusi baada ya Urusi kuivamilia Ukraine vita ambayo si tu imeleta madhara na maafa kwa Ukraine bali dunia kwa ujumla ikiwemo kupandisha bei za mafuta na chakula. Katika siku hiii tuangalia machache yaliyofanywa na moja tu la mashirika mengi ya Umoja wa Mataifa lile la Mpango wa Chakula duniani WFP katika kuwasaidia wananchi wa Ukraine.

Sauti
3'5"