Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Debora Mtambalika ni mmoja wa wanafunzi katika chuo cha Afrika cha mafunzo ya kutengeneza ndege zisizo na rubani, ADDA nchini Malawi.
© UNICEF/UNI280220

Shukrani kwa UNICEF kutupatia mafunzo ya ndege zisizo na rubani ndani – Vijana Afrika

Miaka miwili na nusu iliyopita, kupitia hapa hapa katika Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa tulikufahamisha kuhusu kuanzishwa kwa shule ya kwanza ya mafunzo kuhusu takwimu na ndege zinazoruka bila rubani (Drone), ADDA ilipofunguliwa nchini Malawi kwa ufadhili wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.  Sasa shule hiyo inaendelea vizuri na wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali wanaosoma hapo wanaushukuru Umoja wa Mataifa kwa kuwafanikishia elimu hii muhimu itakayosaidia katika maendeleo ya jamii za sasa na kwa siku zijazo.

Sauti
2'39"
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakisindikiza wapiganaji wa M23 waliojisalimisha Kivu Kaskazini. (MAKTABA)
MONUSCO

Uchunguzi kuhusu askari wa MONUSCO kuhusika katika tukio baya la mauaji DRC unaendelea 

Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akizungumza na waandishi wa habari hii leo Jumanne, Agosti 2, mjini New York Marekani kuhusu mambo mbalimbali yanayoendelea katika Umoja wa Mataifa, ameeleza kile kinachoendelea hivi sasa kuhusiana na tukio baya la mauaji ya raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC lililohusisha askari wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO katika eneo la Kasindi, mpaka wa Uganda na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.