Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Naibu Mwakilisih wa Katibu Mkuu wa UN nchini DRC Kassim Diagne akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari 26 Julai 2022, mkutano  ulihudhuriwa pia na Msemaji wa Serikali ambaye pia ni Waziri wa Habari Patrick Muyaya.
UN/Boybe Malenga

Vurugu dhidi ya ofisi za UN DRC: Serikali kuwasaka na kuwafikisha mbele ya sheria watuhumiwa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imesihi utulivu miongoni mwa wananchi baada ya maandamano na uvamizi dhidi ya vituo vya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO kwenye miji ya Goma na Butembo jimboni Kivu Kaskazini, tukio ambalo hata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka mamlaka zichunguze na sheria ichukue mkondo wake. Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ana taarifa zaidi.

Sauti
3'22"
Mfanyabiashara barabarani akiuza chakula barani Afrika
IMF

Dunia kushuhudia kudorora zaidi kwa uchumi: IMF

Ripoti ya hali ya uchumi kwa robo ya pili ya mwaka huu wa 2022 ambao ni mwezi Aprili hadi Juni ambayo imetolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF imesema matarajio ya ukuaji wa uchumi duniani yanazidi kukumbwa na kiza na yanakosa uhakika na kwamba matumaini ya uchumi kukwamuka mwaka 2021 yanazidi kuyoyoma mwaka huu wa 2022. 

Sauti
2'34"
Magari haya ya kivita ya kubeba askari wa Tanzania huko DR Congo.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

Uvamizi wa vituo vya UN DRC; Walinda amani 3 wauawa

Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mlinda amani askari wa kulinda amani na polisi  wawili wa Umoja wa Mataifa wameuawa baada ya waandamanaji kuvamia kituo cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO huko Butembo na kupora silaha za polisi wa kitaifa na kuanza mashambulizi.