Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mwanamke akipokea chanjo dhidi ya COVID-19 kama sehemu ya kampeni ya chanjo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNICEF/Zoe Mangwinda

Afrika yaanza kulidhibiti janga la COVID-19: WHO

Afrika iko mbioni kudhibiti janga la COVID-19 mwaka huu ikiwa muelekeo wa sasa utaendelea, lakini itatakiwa kuendelea kuwa makini, amesema mkuu wa ofisi ya kikanda ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO Dokta. Matshidiso Moeti hii leo.

Bernice Armelle Bancole ni mwanasayansi katika Sayansi ya Kilimo. Anatoka Benin. Anataka kusaidia kutokomeza matumizi makubwa ya viua wadudu katika nchi za Afrika.
UNESCO/OWSD

Vijinasaba vya mwili havitofautishi uwezo wa msichana na mvulana kwenye sayansi 

Kuelekea siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi, Tume ya Taifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni, UNESCO nchini Tanzania, imesihi wadau mbalimbali wa masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati nchini humo, STEM wazingatie matamko mbalimbali ya kimataifa kwa lengo la kuhakikisha elimu inachangia katika maendeleo endelevu.

UNMAS imekuwa ikitegua mabomu ya ardhini Sudan Kusini yaliyoachwa kutokana na mgogoro.
UNMAS/Irina Punga

UNMAS yaendelea na juhudi za kutegua mabomu ya ardhini Sudan Kusini ili maisha yaendelee

Raia wa baadhi ya maeneo nchini Sudan Kusini wameendelea kuishi kwa mashaka kutokana na mabomu ya ardhini yaliyoko katika maeneo yao huku hatari zaidi ikiongezek katika msimu wa mvua ambapo maji husogeza mabomu hayo. Timu ya wataalamu kutoka ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuondokana na mabomu ya kutegwa ardhini, UNMAS pamoja na Mamlaka za Kitaifa wanafanya kazi kila siku nchini humo ili kuyadhibiti mabomu ambayo hayajalipuka. 

Sauti
2'6"
Wahamiaji wakisajiliwa katika Kituo cha Usafiri cha Agadez nchini Niger.
IOM

Niger yapongezwa kwa ukarimu kwa wasaka hifadhi na wakimbizi

Viongozi wa mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la Kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi na lile la Uhamiaji IOM Antonio Vittorino wamefanya ziara nchini Niger, huko Agadez ambalo ni eneo la mpito la watu wanaotafuta hifadhi na wahamiaji nchini Niger ambalo limeongezeka kuwa na idadai kubwa ya watu wenye kuhitaji msaada wa usalama na fursa. 

Audio Duration
2'52"