Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Muuguzi akitoa chanjo ya Polio kwa mtoto mchanga katika hospitali nchini Malawi
© UNICEF/Giacomo Pirozzi

Mwongozo mpya wa WHO/ILO kuwalinda wahudumu wa afya

Taarifa ya pamoja iliyotolewa leo na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na lile la kazi duniani ILO imetoa mwongozo mpya kuhusu kuendeleza na kutekeleza mipango imara ya afya na usalama kazini kwa wafanyakazi wa sekta ya afya, wakati huu janga la COVID-19 likiendelea kuwapa shinikizo kubwa wafanyakazi hao.  

Wanawake wanachimba mabwawa ya katikati ya mwezi ili kuokoa maji nchini Niger.
©FAO/Giulio Napolitano

Sahel inakabiliwa na janga kubwa la chakula, aonya mkuu wa WFP

Idadi ya watu walio katika hatihati ya baa la njaa katika eneo la Sahel imeongezeka karibu mara kumi katika miaka mitatu iliyopita na idadi ya watu waliokimbia makazi yao imeongezeka kwa karibu asilimia 400% wakati eneo hilo likikabiliwa na mgogoro mbaya zaidi wa chakula katika zaidi ya muongo mmoja, anaonya mkurugenzi mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani- WFP, David Beasley.