Katu kambi za wakimbizi wa ndani hazipaswi kushambuliwa na kuporwa- UN
Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu nchini Sudan, Gwi-Yeop Son amelaani vikali mashambulizi dhidi ya ofisi za kibinadamu na uporaji wa mali na vifaa kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kalma huko Nyala Darfur kusini.