Vizuizi visivyo rasmi vyadororesha biashara Afrika Mashariki
Matumaini yanaelekezwa Kigali Rwanda ambako nchi za Afrika zinatarajiwa kutia saini makubaliano ya eneo la biashara huru na hivyo kupanua wigo wa soko la bidhaa barani humo.
Matumaini yanaelekezwa Kigali Rwanda ambako nchi za Afrika zinatarajiwa kutia saini makubaliano ya eneo la biashara huru na hivyo kupanua wigo wa soko la bidhaa barani humo.
Mkutano wa 62 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani, CSW62 umeanza makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kubwa zaidi linaloangaziwa ni wanawake na wasichana wa vijiji. Wawakilishi wa mashirika ya kiraia wamefika na miongoni mwao ni Maria Mamasita kutoka Monduli mkoa wa Arusha nchini Tanzania.
Nchi nyingine za Kiafrika zilizo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe ziige mfano wa Liberia na kumaliza mizozo ili kunusuru raia wake. Ushauri huo umetolewa na Jenerali mstaafu Daniel Opande aliyekuwa kamanda wa kwanza wa kikosi cha kulinda amani nchini Liberia. Alipozungumza na Zipporah Musau wa idara ya mawasiliano ya umma ya umoja wa Mataifa jenerali msattafu Opande asisitiza hata hivyo haikuwa kazi rahisi kufikia muafaka, kuketi pamoja kujadiliana na kudumisha amani ambayo sasa Liberia inajivunia.
Bidhaa za tumbaku zinasababisha madhara mengi sana hususani kiafya. Shirika la afya duniani WHO sasa linataka kila nchi mwanachaka kuchukua hatua madhubuti kudhibiti hali hiyo kwa kuweka sheria na kuzitekeleza.
Lugha ya mama inasalia ndio msingi wa kumwezesha binadamu kujikwamua na maisha yake. Umfundishapo kwa kutumia lugha ya mapokeo atatumia muda mrefu kuelewa lakini ukitumia lugha ya mama uelewa ni wa haraka zaidi na una tija.
Ujumbe wa siku ya radio duniani mwaka huu wa 2018 ni Radio na Michezo! Umoja wa Mataifa unataka chombo hicho adhimu kitumike kusaidia watu kuchanua na kuonyesha uwezo wao wote. Miongoni mwa watu ambao radio imeweza kuibua stadi zao ni Jane John, mtangazaji wa kike wa habari za michezo katika shirika la utangazaji nchini Tanzania, TBC. Assumpta Massoi alizungumza na Jane kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam, Tanzania na kuanza kwa kumuuliza manufaa ya radio!
Nchini Tanzania harakati za shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA zimesaidia kuepusha wanawake na watoto wa kike siyo tu dhidi ya mila hatarishi ya ukeketaji au FGM, bali pia zimesaidia kubadili mtazamo wa wanaume kuhusu kuoa wanawake ambao hawajakeketwa. Ali Haji Hamad, afisa wa jinsia kwenye ofisi hiyo amezungumza na Assumpta Massoi kwa idhaa hii.
Wakazi wa Gazi na Makongeni huko Kwale mjini Mombasa nchini Kenya waliamua kushikamana na kulivalia njuga suala la uhifadhi wa mazingira kwa kuanzisha mradi ambao pia unawakwamua katika umasikini.