Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Penye nia pana njia- Mikoko Pamoja

Josephat Mwamba Mtwana na Fatuma Zuga Abddallah wakati wakihojiwa na Idhaa ya Kiswahili baada ya kushinda tuzo yao ya Equator inayotolewa na UNDP

Mikoko ni miti muhimu sana lakini kwa muda mrefu wanajamii wamekuwa wakiikata na kuitumia kwa shughuli mbalimbali ikiwemo ujenzi.

UN News Kiswahili
Josephat Mwamba Mtwana na Fatuma Zuga Abddallah wakati wakihojiwa na Idhaa ya Kiswahili baada ya kushinda tuzo yao ya Equator inayotolewa na UNDP

Penye nia pana njia- Mikoko Pamoja

Tabianchi na mazingira

Wakazi wa Gazi na Makongeni huko Kwale mjini Mombasa nchini Kenya waliamua kushikamana na kulivalia njuga suala la uhifadhi wa mazingira kwa kuanzisha mradi ambao pia unawakwamua katika umasikini.

Mradi huo ujulikanao kama "Mikoko Pamoja" ni wa kwanza kuendeshwa na jamii barani Afrika na umejikita katika upandaji wa mikoko ambayo inatoa hewa ya ukaa.

Wana mradi wanaikusanya na kuiuza katika makampuni na watu binafsi na fedha wanazopata zinawanufaisha wanajamii. Miongoni mwa wana mradi hao ni Bi Hafsa Mohamed Zuga na bwana Josephat Mwamba Mtwana walipata fursa ya kuzumza na Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili kuhusu mradi wao