Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mangariba wadondosha nyembe zao Tanzania, wanaume nao wafungua masikio

Mwanamke akiwa ameshikilia kisu kilichotumika kwenye ukeketaji.

Awali programu nyingi kuhusu FGM zilionekana kuhusu wanawake pekee, lakini sasa UNFPA imekuwa na programu zinazojumuisha pia wanaume.

UNICEF/Catherine Ntabadde
Mwanamke akiwa ameshikilia kisu kilichotumika kwenye ukeketaji.

Mangariba wadondosha nyembe zao Tanzania, wanaume nao wafungua masikio

Utamaduni na Elimu

Nchini Tanzania harakati za shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA zimesaidia kuepusha wanawake na watoto wa kike siyo tu dhidi ya mila hatarishi ya ukeketaji au FGM, bali pia zimesaidia kubadili mtazamo wa wanaume kuhusu kuoa wanawake ambao hawajakeketwa. Ali Haji Hamad, afisa wa jinsia kwenye ofisi hiyo amezungumza na Assumpta Massoi kwa idhaa hii.

Maswali ambayo yameulizwa.

  1. Hali ya ukeketaji nchini Tanzania hivi sasa iko vipi?
  2. Nini hasa kichocheo cha mafanikio hayo?
  3. Maghariba imekuwa ni vigumu sana kuachia zana zao kwa kuwa ni mbinu ya kujipatia kipato. Nini kimefanyika?
  4. Bila kukeketwa wasichana wanaona aibu kuolewa na wavulana wanaona aibu kuoa mwanamke hajakeketwa. Nini kimefanyika kubadili mtazamo?