Mangariba wadondosha nyembe zao Tanzania, wanaume nao wafungua masikio
Utamaduni na Elimu
Nchini Tanzania harakati za shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA zimesaidia kuepusha wanawake na watoto wa kike siyo tu dhidi ya mila hatarishi ya ukeketaji au FGM, bali pia zimesaidia kubadili mtazamo wa wanaume kuhusu kuoa wanawake ambao hawajakeketwa. Ali Haji Hamad, afisa wa jinsia kwenye ofisi hiyo amezungumza na Assumpta Massoi kwa idhaa hii.
Maswali ambayo yameulizwa.
- Hali ya ukeketaji nchini Tanzania hivi sasa iko vipi?
- Nini hasa kichocheo cha mafanikio hayo?
- Maghariba imekuwa ni vigumu sana kuachia zana zao kwa kuwa ni mbinu ya kujipatia kipato. Nini kimefanyika?
- Bila kukeketwa wasichana wanaona aibu kuolewa na wavulana wanaona aibu kuoa mwanamke hajakeketwa. Nini kimefanyika kubadili mtazamo?