Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukraine

Mtoto Alex akiw akwenye mashine ya kumsaidia kupata hewa ya oksijeni katika kituo cha watoto wachanga, Ukraine.
Vayu Global Health/Unitaid

Mashine za kusaidia watoto kupumua zapelekwa Ukraine; ni ubunifu kutoka Kenya

Mashine 220 za kusaidia watoto wachanga kupata hewa ya oksijeni kutokana na kuwa hatarini kufariki dunia baada ya kuzaliwa ambazo zimetengenezwa nchini Kenya kwa msaada wa shirika la Umoja wa MAtaifa la kufanikisha upatikanaji wa dawa na tiba kwa gharama nafuu UNITAID zimepelekwa nchini Ukraine wakati huu ambapo vita vinakwamisha huduma za uzazi na kujifungua. 

Sauti
2'3"
Mama na mwanae wakiondoka kituo cha treni cha Lvivi nchini Ukraine.
© UNICEF/Giovanni Diffidenti

Mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani Ukraine:IOM

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM inasema mtu 1 kati ya 6 ni mkimbizi wa ndani nchini  Ukraine na hivyo kuifanya idadi ya watu waliokimbia makazi yao na kusalia wakimbizi wa ndani tangu kuanza kwa mzozo wa Ukraine tarehe 24 mwezi Februari mwaka huu kufikia zaidi ya watu milioni 7.7 sawa na asilimia 17 ya watu wote wa taifa hilo.

Sauti
1'59"