Heko wanaojitolea kusaidia wengine hata wenyewe wakiwa kwenye shida- Guterres
Hii leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya utoaji wa misaada ya kibinadamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amepazia sauti watoa huduma za kibinadamu ambao hufanya kazi kutwa kucha ili dunia iwe pahala bora hasa wale wanaopitia majanga wanaojikuta wao wenyewe wakibeba jukumu la kutoa msaada.