Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Wanawake wa Ukraine, wanaokimbia mzozo wakisubiri lifti ili kufikia kituo cha wakimbizi nchini Poland.
© Daniele Aguzzoli
Wanawake wa Ukraine, wanaokimbia mzozo wakisubiri lifti ili kufikia kituo cha wakimbizi nchini Poland.

WHO yatoa huduma za matibabu na usaidizi wa kisaikolojia kwa wakimbizi wa Ukraine

29 Machi 2022
Msaada wa Kibinadamu

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limejizatiti kuhakikisha wakimbizi kutoka Ukraine wanapatiwa msaada wa huduma za matibabu na usaidizi wa kisaikolojia.

"Nipo peke yangu, nipo pekeyangu" ndivyo alivyosema Valentina mwenye umri wa miaka 67 aliyewasili kwenye kituo cha wakimbizi cha Horodlo nchini Poland akitokea Bila Tserkva nchini Ukraine akikimbia vita inayoendelea nchini mwake.

Valentina aliugua polio tangu angali mdogo na hivyo ana ulemavu wa kutembea.

Safari ya kutoka Ukraine ilikuwa ngumu, alisafiri kwa siku tatu hadi kufika kituoni. Alilazimika kubebwa kutoka gari moja hadi jingine.

Sasa ameshaonana na daktari aliyempatia dawa za maumivu huku akimsubiri binti yake amchukue kwenda kuishi naye nchini Israel.
Beate Sawicka ni muuguzi kwa zaidi ya miaka 34 nchini Poland, anayefanya kazi katika kituo chakupokea wakimbizi cha Dorohusk na anasema sasa idadi ya wazee ni kubwa na wana magonjwa sugu. Pia kuna watu wenye ulemavu, tofauti na hapo awali walikuwa wakipokea wakina mama na watoto.

“Moyo wangu unavunjika kuwaona wakiwa katika hali hii. Wao sio wagonjwa tu, bali pia wamechoka, wamechoka sana, wanatokwa machozi. Tunajaribu kuwasaidia iwezekanavyo. Kuna baadhi yao inabidi tuwabadilishe nepi wakiwa wamekaa kwenye viti mwendo ili tusiwazungushe sana. Nimeifanya kazi hii ya uuguzi kwa miaka 34. Nimekuwa nikihudumia wagonjwa wa aina hii lakini hali zao zinazofaa wawe hospitalini. Hapa kuna baridi, wachafu, kwa sababu wanasafiri kwa saa 48. Moyo wangu unapasuka, hali inatisha kwa tunachokiona hapa.”

Nako katika eneo la Krowico Sama Mtaalamu wa afya ya akili na msaada wa kisaikoloji na jamii wa WHO Selma Sevkli, anazungumza na Olga, msichana mwenye umri wa miaka 20 mwanafunzi wa mwaka wa kwanza Chuo Kikuu nchini Ukraine aliyekuwa anasomea udaktari lakini sasa anaona ndoto zake zimezimika.

“Unachojisikia, unachopitia ni kawaida sana. Huenda nyakati fulani ukahisi: ‘Kwa nini sina nguvu?’, ‘Ni nini kitakachotokea?’, unakuwa na uoga, yote hayo ni ya kawaida sana. Kila mtu anapitia jambo lile lile. Hivi sasa jaribu kuwa na utulivu. Umezungukwa na watu wengi wenye mioyo mizuri ambao wanajaribu kuwasaidia kutoka kote ulimwenguni. Kila mtu anajaribu kusaidia.

Olga akizungumza na mtaalamu wa WHO amesema wanahitaji msaada wa kisaikolojia kwa hali na mali kwa kuwa watu wengi wamechanganyikiwa na wamepoteza matumaini akitolea mfano mama yake ambaye amekuwa akilia muda wote na kuangalia habari kwenye simu yake ya mkononi huku mdogo wake akiwa hataki kabisa kucheza au kujihusisha na mtu yeyote na akitaka jambo moja tu, kurudi nyumbani.

WHO imeeleza kuwa lengo lao ni kuhakikisha wanaandaa usaidizi sio tu katika vituo ya kuwapokea wakimbizi wanaoingia nchini Poland bali wanahakikisha wakimbizi hao wanapata usaidizi unaohitaji wa afya ya akili na mahitaji mengine katika maeneo wanayoelekea baada ya kuondoka kituoni hapo.

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
Msaada kwa wakimbizi

SIKILIZA RADIO YA UMOJA WA MATAIFA

    Taarifa Zihusianazo

    Ghada Krayem, mkimbizi wa kipalestina, akipokea mafunzo ya ufundi wa umeme wa jua katika kituo cha GTC

    Marekani kutoa milioni 135.8 kusaidia wakimbizi wa kipalestina

    Wakati machafuko yakishika kasi Ukraine watu wamesongamana kwenye kituo cha tren Lviv wakisubiri kusafirishwa kwenda Poland

    UN yashtushwa na athari za kibinadamu katika miji iliyozingirwa Ukraine

    Jengo la makazi lililoharibiwa na operesheni za kijeshi zinazoendelea huko Kyiv, Ukraine, tarehe 26 Februari 2022.

    Kila siku ya vita Ukraine, ni dalili ya kutumbukiza taifa hilo kwenye lindi la umaskini- UNDP

    Maktaba

    • Taarifa kwa watangazaji
    • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
    • Angalizo
    • UN Journal
    • Taarifa za Habari
    • Mikutano
    • Maktaba ya Picha na Video
    • Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu

    • Taarifa zote
    • Safari za kiofisi
    • Kona ya wanahabari
    • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

    Msemaji wa UN

    • Nyaraka zote
    • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
    • Maandishi ya mkutano na wanahabari
    • Taarifa kwa wanahabari

    Tupate

    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • RSS
    • Mawasiliano
    • Rambaza
    • Washirika wetu kwa sasa
    Umoja wa Mataifa
    Changia
    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • Soundcloud
    • Podcast
    • UN Social Media
    • A-Z Site Index
    • Hakimiliki
    • Maswali ya mara kwa Mara
    • Fraud Alert
    • Privacy Notice
    • Kanuni za matumizi
    • Facebook
    • Twitter
    • YouTube
    • SoundCloud
    • Podcast
    • More Socials