Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sudan Kusini

Michael Dunford, Mkurugenzi wa WFP Pembe ya Afrika akihojiwa na UN News.
UN/ Leah Mushi

Hatari ya baa la njaa bado ni jinamizi linaloizonga Somalia: WFP Dunford

Ukame uliolighubika eneo la Pembe ya Afrika kwa miongo minne mfululizo umesababisha changamoto kubwa kwa mamilioni ya raia wa Kenya, Ethiopia na Somalia nchi ambayo maeneo mengi yanakabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula na hatihati ya kutumbukia kwenye baa la njaa. Mashirika ya misaada ya kibinadamu likiwepo la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yako mstari wa mbele kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani wa chakula.

Sauti
2'
Soko nchini Sudan Kusini
© UNICEF/Sebastian Rich

UNMISS yapatia mafunzo wafanyabiashara Sudan Kusini ili wafanye biashara kwa ufanisi

Ushirikiano na ukuaji kiuchumi ni miongoni mwa masuala muhimu katika kuhakikisha nchi yoyote ina amani na wananchi wake wanapata Maendeleo. Na ili kuhakikisha wananchi wa Sudan Kusini wana amani na maendeleo, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda Amani nchini humo UNMISS umeandaa warsha ya biashara lengo likiwa ni kuwatia moyo wafanyabiashara wa ndani na kuwawezesha kiuchumi ili nao waweze kuimarisha biashara zao lakini pia waweze kufanya biashara na Umoja wa Mataifa .

Sauti
3'34"
Sidonie, mwenye umri wa miaka 10, akiwa mbele ya darasa la shule yake ya msingi Kitambo iliyoko mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Kinshasa.
© UNICEF/Josue Mulala

Elimu ya sasa inapitia janga kubwa: Tuirekebishe kwa mustakabali wa watoto

Ingawa msemo wa haki ya binadamu umezoelekea, hakuna haki ya binadamu yoyote ambayo imetolewa bure bila kupiganiwa, vivyo hivyo inapaswa kuwa kwa elimu, amesema Leonardo Garnier, Mshauri Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mkutano wa Ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu duniani, mkutano unaoanza Ijumaa hii kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Kufahamu msingi wa kauli hiyo, 

Sauti
2'
Kambini Kakuma
UN/Esperanza Tabisha

Wakimbizi tukikirimiwa tunarejesha fadhila kwa jamii:Bahati, Micheline na Agnes

Kutana na wakimbizi Bahati Hategekimana kutoka Rwanda, Micheline Muhima kutoka Uganda na Agnes Mude kutoka Sudan Kusini ambao wote walikuwa wakiishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya, lakini sasa kupitia mradi wa majaribio wa kuthamini mchango wa wakimbizi EMPP, unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, mjini Pictou na serikali ya Canada watatu hao si wakimbizi tena bali ni wafanyakazi wa huduma ya jamii kwenye kituo cha Glen Haven Manor kilichopo jimboni Nova Scotia nchini Canada. 

Sauti
2'34"