Bila mafuta, hakuna mkate: WFP
Hali mbaya inayowakabili mamia kwa maelfu ya Wapalestina huko Gaza inaweza kuwa mbaya zaidi, kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta ambao unatishia kusimamisha chakula na shughuli zingine za kibinadamu.
Hali mbaya inayowakabili mamia kwa maelfu ya Wapalestina huko Gaza inaweza kuwa mbaya zaidi, kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta ambao unatishia kusimamisha chakula na shughuli zingine za kibinadamu.
Mratibu wa mwasuala ya kibinada wa Umoja wa Mataifa kwenye eneo linalokaliwa la Palestina Lynn Hastings amesema Gaza imepoteza mawasiliano na Dunia wakati kukiwa na tarifa za kushamiri kwa mashambulizi ya mabonu.
Hebu vuta tasirwa, mama akiwabembeleza watoto wake usiku, hofu ya kutengana nao ikija kama kivuli, kujaribu awezavyo kujilinda yeye na familia yake, ili ‘wasiwe kumbukumbu’ hata hivyo, hadithi yetu ni kumbukumbu tu sasa, lakini wakati ujao bado haujaandikwa, nikiamka kesho, nataka hili limalizike, ilinirejee mahali patakatifu, kwenye nyumba yetu.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa llimepiga kura kupitisha azimio la kulinda raia kwenye mzozo unaoendelea baina ya Israel na Palestina huku katika kikao cha 10 cha dharura ambacho kimefanyika leo kwa siku ya pili kuhu kukiwa na mvutano kwenye Baraza la Usalama na hali katika eneo linalozingirwa la Gaza ikizidi kuwa mbaya.
Hali Mashariki ya Kati inazidi kuwa mbayá. Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo amezisihi pande zote katika mzozo kusitisha uhasama , huku mashirika ya misaada yakionya kuhusu janga kubwa zaidi la kibinadamu, wakati hapa Makao Makuu kikao cha 10 cha dharura kuhusu mzozo huo wa Mashariki ya Kati kikiendelea leo.
Wataalam wa afya wa Israel wanafanya kazi usiku kucha kufuatia mashambulizi ya tarehe 7 October la kikundi cha wanamgambo wa Kipalestina cha Hamas ambayo yaliua watu 1,400 na kujeruhi zaidi ya 4,600 kulingana na Mwakilishi wa shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO nchini Israel, Michael Thieren.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo mjini New York, limeitisha mkutano maalum wa dharura kuhusu mzozo baina ya Israel na Gaza, huku kukiwa na mkwamo unaoendelea katika Baraza la Usalama, na hali katika eneo hilo inazidi kuwa mbaya zaidi kila saa.
Operesheni za kibinadamu huko Gaza zimekuwa hatarini kusitishwa leo Jumatano kutokana na changamoto kubwa ya mafuta inayoendelea, wakati Israeli ikiendelea kukabiliana na mgogoro wa muda mrefu wa mateka huku kukiwa na athari mbaya ya mashambulizi ya Hamas ya Oktoba 7.
Mashirika ya Umoja wa Mataifa yataka misaada zaidi ikiwemo mafuta kuingia Gaza, Leo ni siku ya Umoja wa Mataifa na Theluthi mbili ya watoto wakimbizi waandikishwa shule Armenia
Idadi ya watu waliouawa huko Gaza imefikia 5,087 kulingana na ripoti zilizotolewa leo na punde kutoka kwa mamlaka za huko, huku kukiwa na mashambulizi ya anga ya Israel kujibu mashambulizi ya Hamas, na wasaidizi wa kibinadamu wakirudia wito wa dharura wa kusitishwa kwa mapigano na misafara zaidi ya misaada kuingia katika Ukanda wa Gaza.