Gaza : ICJ imeitaka Israel kukomesha mashambulizi dhidi ya Rafah mara moja
Mahakama ya kimataifa ya haki ICJ leo imetoa maamuzi ya kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel iliyowasilishwa Mei 10 ikiitaka ICJ kuiamuru Israel isitishe mara moja oparesheni zake zote za kijeshi na kuwezesha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu. Na tarehe 16 na 17 Mei,kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Kuzuia na Kuadhibu Uhalifu wa Mauaji ya Kimbari katika Ukanda wa Gaza.