Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashariki ya Kati

Chumba cha Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ, huko The Hague katika kesi ya Afrika Kusini dhidi ya sraeli.
© ICJ/Wendy van Bree

Gaza : ICJ imeitaka Israel kukomesha mashambulizi dhidi ya Rafah mara moja

Mahakama ya kimataifa ya haki ICJ leo imetoa maamuzi ya kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel iliyowasilishwa Mei 10 ikiitaka ICJ kuiamuru Israel isitishe mara moja oparesheni zake zote za kijeshi na kuwezesha upatikanaji wa misaada ya kibinadamu. Na tarehe 16 na 17 Mei,kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Kuzuia na Kuadhibu Uhalifu wa Mauaji ya Kimbari katika Ukanda wa Gaza.

Audio Duration
1'54"
Familia huko Gaza zinatatizika kupata chakula cha kutosha.
© WFP/Ali Jadallah

Baada ya kulazimishwa kuondoka Rafah baadhi ya wapalestina warejea kwenye nyumba zao zilizoathiriwa na mabomu

Kuongezeka kwa shughuli za kijeshi huko Rafah, kusini mwa Gaza, kumesababisha mamia kwa maelfu ya watu kuyahama makazi yao, na kufanya maisha kuwa magumu zaidi kwa maelfu ya familia ambazo tayari zimelazimika kuyahama makazi yao mara kadhaa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP lina wasiwasi mkubwa kwamba hali hii ya kuhama hama inaweza kusababisha janga la kibinadamu, nakupelekea kusimama kwa shughuli za kutoa misaada ya kibinadamu.

Sauti
2'32"
Kaskazini mwa Gaza iko kwenye magofu baada ya miezi kadhaa ya mashambulizi ya mabomu.
© WFP/Ali Jadallah

Wananchi wa Gaza wako katika jakamoyo wakisubiri taarifa kuhusu wito wa kusitisha mapigano: UN

Wakati kukiwa na ongezeko la wito wa kimataifa kwa Israel kujizuia na mashambulizi zaidi Gaza na ripoti za leo za mashambulizi mengine mabaya zaidi ya usiku kucha, wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamesisitiza kuhusu athari mbaya zinazoendelea za vita hiyo na haja ya kuhakikisha njia za kuaminika za usambazaji wa misaada kwa watu wanaohitaji kwa udi na uvumba zinapatikana. 

Sauti
1'57"
Uopoaji wa miili kutoka chini ya vifusi vya nyumba katika kitongoji cha Al-Nasr, mashariki mwa mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.
UN News/Ziad Taleb

Baraza la Usalama kujadili ombi la Palestina kuwa mwanachama wa UN

Huko Gaza, watoa misaada ya kibinadamu wakiwa na wasiwasi mkubwa juu ya mipango ya Israel kuvamia eneo la Rafah hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa Palestina imeanza mchakato wa kuwa mwanachama rasmi wa Umoja wa Mataifa kwani hivi sasa ujumbe wake ni uangalizi usioipatia hadhi ya kupiga kura. Mchakato huo unaanzia ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. 

Sauti
2'24"
Mvulana anakimbia katika mitaa iliyoharibiwa ya Gaza.
© UNRWA/Ashraf Amra

GAZA: Miezi 6 ya mzozo Guterres akemea matumizi ya Akili Mnemba

Kesho kutwa jumapili ikiwa ndio itatimu miezi sita ya mzozo wa Gaza, huko Mashariki ya Kati, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani akirejelea wito wake wa sitisho la mapigano kwa misinigi ya kiutu, kuachiliwa kwa mateka wote bila masharti, ulinzi wa raia na misaada ya kiutu ifikie walengwa bila vikwazo vyovyote huku akikgusia pia Israeli kutumia akili mnemba kwenye operesheni zake. 

Sauti
2'40"