Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Bendera ya Umoja wa Mataifa ikikabidhiwa kwa maafisa wa MONUSCO nchini DRC kuashiria kufungwa kwa ofisi ndogo za ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani kwenye eneo hilo lililoko kilometa takribani 140 kutoka mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.
UN/George Musubao

Ofisi ya MONUSCO Lubero, Kivu Kaskazini yafungwa

DRC, MONUSCO umefunga kituo chake kilichoko Lubero jimboni Kivu Kaskazini baada ya kuweko huko kwa miaka 21.Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wake wa kujiondoa kwa utaratibu kutoka DRC, kwa mujibu wa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufuatia ombi la serikali ya DRC.

Afisa Habari wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO ofisi ya Beni jimboni Kivu Kaskazini akipatia mafunzo wanahabari, wanaharakati na wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuhusu habari potofu na habari za uongo mjini Beni.
UN./George Musubao

MONUSCO imetuepusha kutumbukia kwenye usambazaji wa habari za uongo na potofu- Wanufaika

Kesho nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ni uchaguzi mkuu ikiwa ni tamati ya kampeni huku Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umeshiriki kwa kusafirisha sio tu vifaa vya uchaguzi lakini pia kuelimisha wananchi jinsi ya kukabili na kuzia habari potofu na za uongo kwani ni tisho la amani na usalama. 

Kikundi Cha Bendera cha Pamoja cha Walinda Amani wa Tanzani na Nepali wakitoa Salamu kwa Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO.
MONUSCO

Walinda amani wa MONUSCO kutoka nchini Tanzania na Nepal watunukiwa Nishani

Vikosi vya Walinda Amani kutoka Tanzania Kwa kushirikiana Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Nepali wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo – DRC wamefanya gwaride la pamoja na kutunikiwa Nishani za Umoja wa Mataifa na Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani DRC, MONUSCO Luteni Jenerali Otavio Miranda Filho ikiwa ni kuthamini mchango wao wa kuhakikisha Amani ya Kudumu na Usalama vinapatikana nchini DRC.

Ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini DRC ilitumia wiki ya Umoja wa Mataifa iliyoenda sambamba na siku ya UN kuonesha kazi za mashirika ya chombo hicho.
UN/Byobe Malenga

UN isisubiri siku yake tu ndio ielezee shughuli zake- Wadau DRC

Mwaka huu wa 2023, tarehe 24 mwezi Oktoba, Umoja wa Mataifa umetimiza miaka 78 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1945 huko San Fransisco nchini Marekani.  Chata ya kuanzisha umoja huo unaupatia majukumu makuu manne ambayo ni Kuendeleza amani na usalama duniani, kusongesha uhusiano wa kirafiki baina ya nchi, kufanikisha ushirikiano wa kimataifa na kuwa kitovu cha kuratibu vitendo vya mataifa.