Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Hisia za wakimbizi nchini Uganda kufuatia mlipuko wa Corona unaoshuhudiwa duniani kote
Katika makala ya wiki hii tutakuwa nchini Uganda tukiangazia shaka na shuku miongoni mwa wakimbizi na hatua za Umoja wa Mataifa wakati huu wa maambukizi ya Corona.
Mwandishi wetu wa Uganda, John Kibego alikwenda kambi ya wakimbizi ya Kyangwali kusikiliza shaka na shuku zao kuhusu hofu ya kuingia kwa virusi vya corona kwenye taifa hilo ambalo bado halina mgonjwa hadi leo Ijumaa.
Mahitaji ya wanawake yapatiwe kipaumbele wakati wa COVID-19: UN Women
Wakati janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 likiendelea kutikisa duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia masuala ya wanawake, UN Women linashirikiana na wadau wake kuhakikisha kuwa madhara ya ugonjwa huo katika jinsia yanaepukika.
UN, mdau wa Kenya katika vita dhidi ya COVID-19: Mratibu Mkazi Kenya
Umoja wa Mataifa unashirikiana kwa karibu na serikali ya Kenya kusaidia kuzuia kusambaa kwa virusi vya Corona, au COVID-19.
Na Siddharth Chatterjee, Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Kenya
Mshikamano, matumaini na ushirikiano vyahitajika kukabili COVID-19: Guterres
Wakati hofu ikiendelea kutanda kote duniani kufuatia kusambaa kwa mlipuko wa virusi vya Corona, COVID-19 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “sasa kuliko wakati mwingine wowote tunahitaji mshikamano, tumaini na utashi wa kisiasa ili kukabiliana na janga hili kwa pamoja.”
Afrika ni wakati wa kuamka na kujiandaa na zahma ya COVID-19:WHO
Shirika la afya ulimwenguni WHO limetoa wito kwa bara la Afrika kuamka na kujiandaa na tishio kubwa la kimataifa za mlipuko wa virusi vya Corona , COVID-19. Katika mkutano wa kila siku na waandishi wa habari mjini Geneva mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt. Tedros Adhamon Ghebreyesus amesema “kitu muhimu na bora kwa Afrika ni kujiandaa kwa zahma na kujiandaa sasa”
Uelewa wa COVID-19 na mbinu za kujikinga miongoni mwa wakazi, Pangani, Tanzania
Wakati visa vya ugonjwa wa COVID-19 vikiongezeka duniani kote na sasa pia Afrika Mashariki ikiwemo nchini Tanzania. Je wananchi wanaelewa vipi kuhusu virusi vya coroan na wamechukua hatua zipi kujikinga dhidi ya virusi hivyo? Tuungane na Saa Zumo wa Redio washirika Pangani FM ambaye amepita katika mitaa ya Pangani mkoani Tanga kusikia maoni ya wananchi kuhusu ugonjwa wa COVID-19 au virusi vya corona.
Tuko pamoja na serikali ya Sudan Kusini katika vita dhidi ya COVID-19:UN
Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini umetangaza hatua mpya katika kusaidia juhudi zinazoongozwa na serikali ya Sudan kusini katika kuzuia na kujiandaa na mlipuko wa virusi vya Corona, COVID-19. Grace Kaneiy ana ripoti kamili.
Taarifa iliyotolewa na Umoja wa Mataifa hii leo nchini humo imesema hatua hizo zinalenga kuwalinda watu wa Sudan Kusini na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa.
Tanzania visa vya COVIDI-19 vyaongezeka, wafanyabiashara wateta
Nchini Tanzania maambukizi ya virusi vya Corona au COVID-19 yameendelea ambapo hii leo wagonjwa wapya wawili wote wakazi wa Dar es salaam wamethibitishwa kuwa na virusi hivyo baaada ya mmoja kuingia nchini kutoka safari ya Denmark, Uswisi na Ufaransa huku mwingine akiwa amerejea kutoka Afrika Kusini. Wagonjwa wote hao sasa wako chini ya uangalizi.
Uganda yajihadhari kabla ya shari ya COVID-19
Serikali ya Uganda imechukua hatua ya kufunga shule zote, masoko na mijumuiko yote ya umma kama mojawapo ya njia za kuzuia kuenea kwa virusi vya corona au COVID-19 kwenye nchi hiyo ambayo yenyewe hadi sasa haina mgonjwa hata mmoja lakini imezungukwa na nchi mlimothibitishwa mlipuko wa virusi hivyo. Kutoka Uganda mwandishi wetu John Kibego anaripoti zaidi.
Hiyo ni sauti ya Rais Wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni akihutubia taifa kuhusu tishio la mlipuko wa virusi hatari vya COVID-19 akiwa kwenye ikulu ya Entebbe.
19 MACHI 2020
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea
-Licha ya kutokuwa na mgonjwa hata mmoja wa COVID-19 serikali ya Uganda imefunga shule zote hadi vyuo vikuu katika maandalizi ya kupambana na mlipuko endapo utazuka ugonjwa huo
-Nchini Sudan Kuisni Umoja wa Mataifa umechukua hatua madhubuti kuisaidia serikali maandalizi ya vita dhidi ya COVID-19 kwa umma na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa kupitia hatua kadhaa