19 MACHI 2020
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea
-Licha ya kutokuwa na mgonjwa hata mmoja wa COVID-19 serikali ya Uganda imefunga shule zote hadi vyuo vikuu katika maandalizi ya kupambana na mlipuko endapo utazuka ugonjwa huo
-Nchini Sudan Kuisni Umoja wa Mataifa umechukua hatua madhubuti kuisaidia serikali maandalizi ya vita dhidi ya COVID-19 kwa umma na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa kupitia hatua kadhaa
-Nako nchini Tanzania wafanyabiashara ndogondogo waelezea mlipuko huu wa COVID-19 unamaanisha nini kwao na athari zake wakati nchi hiyo ikitangaza idadi ya wagonjwa kufikia 6.
-Makala yetu leo inatupeleka wilayani Pangani Tanga Tanzania kusikia maoni ya wananchi kuhusu COVID-19
-Na mashinani leo utasikia ujumbe wa shirika la afya duniani WHO ulifafanua je uvae barakoa ya kitabibu katika kujikinga na COVID-19 na uvae vipi.