Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
27 APRILI 2020
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Watoto wengi wakosa chanjo hata kabla ya kuzunga kwa janga la virusi vya Corona au COVID-19 limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF likitaka hatua madhubuti zichukuliwe sasa kuhakikia watoto wanapata chanjo zote
-Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF leo limeanza kusambaza mashine za hewa ya Oxygen katika vituo sita vya afya vinavyohudumia wagonjwa wa COVID-19
UNICEF yagawa mashine 32 za Oksijeni DRC kupambana na COVID-19
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia latoto UNICEF limesambaza mashine 32 za hewa ya Oksijeni ili kusaidia wagonjwa mahututi katika vita dhidi ya janga la virusi vya Corona au COVID-19 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC
Unyanyapaa ni changamoto kubwa katika vita dhidi ya COVID-19 Uganda
Suala la unyanyapaa wa aina yoyote ile ni mtihani mkubwa katika jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa ambao hutoa wito kila uchao kuhakikisha changamoto hiyo inatokomezwa .Wakati huu wa mlipuko wa janga la virusi vya Corona au COVID-19 unyanyapaa umeelezwa kujitokeza na kusababisha changamoto kwa wagonjwa na washukiwa na hata kuwafanya wengine kutojitokeza kufanya vipimo hali ambayo shirika la afya ulimwenguni WHO limeonya kuwa ni hatari kubwa na kikwazo cha kupambana na ugonjwa huo.
24 APRILI 2020
Katika Jarida la Habari hii leo Flora Nducha anakuletea
-Mwezi mtukufu wa Ramadhani unaanza leo kote duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa awatakia kila la heri Waislam wote na kusema kwamba COVID-19 itaifanya Ramadhan ya mwaka huu kuwa tofauti kabisa
-Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amesema anatiwa hofu na kamatakamata na kubanwa kwa vyombo vya habari wakati huu wa janga la COVID-19 ambapo taarifa sahihi ni muhimu sana
Ushirikiano wa kimataifa wazinduliwa kufanya chanjo na tiba ya COVID-19 kupatikana kwa wote
Mkakati mpya wa kimataifa umezinduliwa leo ili kusongesha mbele juhudi za maendeleo, uzalishaji na fursa sawa ya nyenzo mpya za kukabiliana na janga la virusi vya corona au COVID-19 hasa katika upatikanaji wa chanjo.
Mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani mwaka huu ni tofauti kabisa- Guterres
Waumini wa dini ya kiislamu ulimwenguni wakianza kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa ujumbe wake wa kuwatakia heri katika mfungo wa sasa ambao amesema ni tofauti kabisa na mingine iliyotangulia kwa ajili ya janga la COVID-19.
Kwa kila siku inayopita, athari za janga la COVID-19 na matokeo yake ni dhahiri :UNFPA
Kwa kila siku inayopita, athariza janga la COVID-19 na matokeo yake ni dhahiri :UNFPA
Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani UNFPA , limesema linashikamana na wale wote wanaojitolea na kuwa katika mstari wa mbele kupigana na janga la virusi vya corona au COVID-19: kuanzia kwa wahudumu wa afya na wanaojitolea kusaidia bila malipo.
Nchini Uganda na Afrika Kusini, UN yazindua ombi la ufadhili kupambana na COVID-19
Nchini Uganda, ambako kuna wagonjwa 56 wa COVID-19, Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo, Rosa Malango hii leo amezindua ombi la dharura la dola milioni 316 za Marekani kwa ajili ya kushughulikia janga hili.
Haki za binadamu ziwe muongozo wa vita dhidi ya COVID-19:UN
Umoja wa Mataifa umesisitiza kwamba haki za binadamu zinapaswa kuwa muongozo katika hatua zinazochukuliwa kupambana na janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19.
23 APRILI 2020
Katika jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
Umoja wa Mataifa wasema teknolojia ya mawasiliano imedhihirisha umuhimu wake hasa wakati huu wa janga la virusi vya Corona au COVID-19 na hivyo kuhimiza wasichana wengi wawezeshwe kuingia katika teknolojia hiyo ya ICT
-Vifaa na misaada kutoka kituo kikuu kilichopo Addis Ababa Ethiopia vyaleta mabadiliko kwa maelfu ya watu katika vita dhidi ya COVID-19 limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP