Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 imelazimu kubadili mfumo wa kazi za uandishi wa Habari
Janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19 limelazimisha tasnia ya Habari kufanyia mabadiliko utendaji wake ili kwenda sanjari na hali halisi hasa ukizingatia hivi sasa , shirika la afya duniani WHO linasisitiza hali ya kutochangamana ili kuepusha maambukizi zaidi. Je Afrika Mashariki vyombo na waandishi wa Habari wanaendeshaje kazi zao ili kuhakikisha jamii inaendelea kuhabarika wakati huu wa COVID-19? Hilo ndilo tunaloliangazia leo katika mada kwa kina. Ungana na Flora Nducha
Hatua maalum zahitajika kuwalinda wenye ulemavu na COVID-19:Bachelet
Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Msataifa Michelle Bachelet amezitaka nchi kuchukua hatua maalum ili kuwajumuisha watu wenye ulemavu katika vita dhidi ya janga la virusi vya corona au COVID-19.
Janga la COVID-19 ni jinamizi kwa wazee-Guterres
Janga la virusi vya corona au COVID-19 linasababisha hofu isiyoelezeka na madhila kwa wazee kote ulimwenguni.
Tukiaadhimisha siku ya wafanyakazi duniani tuwakumbe wanaobeba mzigo wa COVID-19:Guterres
Katika sehemu mbalimbali duniani leo ni sikukuu ya wafanyakazi, na mwaka huu kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres siku hiyo imeghubikwa na janga la virusi vya corona au COVID-19, na kwa hakika imedhihirisha kwamba kuna wafanyakazi ambao mara nyingi hubeba mzigo mkubwa bila kuonekana.
Miongozo mipya yatolewa kuhusu njia ya ufunguzi salama wa shule hali itakapotengamaa
Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na Benki ya dunia, hii leo mjini New York Marekani, Paris Ufaransa na Roma Italia, wametoa miongozo kuhusu namna salama ya kuzifungua shule kutokana na kufungwa ambako kunawaathiri takribani wanafunzi bilioni 1.3 kote duniani.
Usitishaji uhasama kimataifa, kusaidia wasiojiweza na mikakati ya kujikwamua ndio kipaumbele cha UN:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo Alhamisi ameweka bayana dhimira ya Umoja wa Mataifa ya kutaka kuvishinda vita dhidi ya janga la virusi vya corona au COVID-19 kwa kujikita na mambo matatu muhimu ambayo ni kufikia usitishwaji wa uhasama kimataifa, kuwasaidia wale wasiojiweza na kujiandaa kujikwamua kiuchumi na kijamii kutoka kwenye janga hili.
COVID-19 yazidisha changamoto za chakula Uganda
Njanga la virusi vya corona au COVID-19 limewaacha raia wengi nchini Uganda wakiwa na changamoto ya kipato hali ambayo
imechangia kuongeza changamoto ya uhakika wa chakula. Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego mevinjari katika maeneo
mbalimbali kuangazia changamotot za upatikanaji wa achakula na lishe wakati huu ambapo mamilioni ya wanannchi wa kipato
cha chini wanakabiliwa na hatua za kuzuia maambukizi ya virusi vya corona kwa kutokwenda kazini, kufanya biashara na hata
COVID-19 imetugeuza wafungwa, sina mtandao wa kufuatilia masomo - Mtoto DRC
Watoto nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, hivi sasa licha ya kutokwenda shuleni kutokana na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, wanatumia muda huo kusoma nyumbani, kusaidia kazi sambamba na kuelimisha jamii ili ijikinge na virusi hivyo.
Udaktari ni wito na ukiwa wako huchoki:Dkt. Wambugu
Kazi ya udaktari kama ilivyo ya ukunga au uuguzi ni wito na wakati majanga kama hivi sasa la virusi vya corona au COVID-19 umuhimu wake unakuwa hauna kifani. Kutana na daktari ambaye pampja na wenzae wanafanya kila wawezalo kuwakinda wakimbizi kambini Kakuma Kenya dhidi ya janga hilo.
Miezi mitatu tangu kutangazwa COVID-19 ni janga bado hatukati tamaa- WHO
Ikiwa leo ni miezi mitatu tangu shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, litangaze kuwa ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 ni dharura ya kiafya ya kimataifa, shirika hilo limesema katu halijakata tamaa na halitokata tamaa katika kuhakikisha virusi hivyo vinatokomezwa.