Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 inabadili mfumo wa usafirishaji haramu wa mihadarati :UNODC Ripoti
Ripoti mpya iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu, UNODC imesema janga la virusi vya corona au COVID-19 limeathiri utaratibu wa usafirishaji haramu wa mihadarati hususan kwa njia ya anga na hivyo kuwafanya wasafirishaji haramu kusaka njia mbadala.
Watoto milioni 116 kuzaliwa miezi 9 baada ya COVID-19 kutangazwa janga, je changamoto ni zipi?
Kuelekea siku ya mama duniani tarehe 10 mwezi huu wa Oktoba, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linakadiria kuwa watoto milioni 116 watakuwa wamezaliwa wiki 40 tangu ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 utangazwe kuwa janga la kimataifa tarehe 11 mwezi Machi mwaka huu.
Guterres:Tukihakikisha haki za wenye ulemavu, tunawekeza katika mustakbali wa Pamoja
Katika mazingira ya kawaida watu wenye ulemavu mara nyingi hukosa fursa ya huduma za msingi kama vile elimu, huduma za afya na fursa za kiuchumi au ushiriki katika jamii.
Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika uzinduzi wa sera kuhusu watu wenye ulemavu na janga la corona au COVID-19.
Katika uzinduzi huo Bwana Guteres amesema janga la COVID 19 linaathiri kila nyanja ya jamii zetu na leo hii anaelezea jinsi gani janga hili linavyoathiri watu bilioni moja wenye ulemavu duniani.
06 Mei 2020
Leo katika Jarida la Umoja wa Mataifa tunaangazia habari tofauti kutoka sehemu mbalimbali duniani:
-Tutasikia kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuhusu uzinduzi wa sere za watu wenye ulemavu na janga la corona au COVID-19.
-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linashirikiana na jamii ili kusaidia kuepusha kusambaa kwa ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 hususan kwenye maeneo ya makazi duni huko Kenya.
UNICEF Kenya yaungana na wafanyakazi wa kujitolea kutokomeza Corona
Nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linashirikiana na jamii ili kusaidia kuepusha kusambaa kwa ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 hususan kwenye maeneo ya makazi duni
Tukihakikisha haki za wenye ulemavu, tunawekeza katika mustakbali wa Pamoja:Guterres
Katika mazingira ya kawaida watu wenye ulemavu mara nyingi hukosa fursa ya huduma za msingi kama vile elimu, huduma za afya na fursa za kiuchumi au ushiriki katika jamii.
Uhuru wa vyombo vya Habari ni chachu ya kukabili COVID-19 na taarifa potofu:UN
Waandishi wa Habari ni kitovu cha kukabiliana na mlipuko hatari wa taarifa potofu zinazoambatana na janga la virusi vya corona au COVID-19 amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Msataifa leo katika mazungumzo kwa njia ya mtandao ya kuchagiza uhuru wa vyombo vya Habari wakati huu wa mgogoro wa kimataifa.
Chama cha wakunga Tanzania tunawashauri wakunga wote kutumia vifaa vilivyotakaswa wakati huu wa COVID-19:Lucy Mabada
Dunia ikielekea kuadhimisha siku ya wakunga hapo kesho tarehe 5 Mei, Chama cha wakunga Tanzania (TAMA) kimewapa ushauri wakunga wote kuzingatia kuvaa vifaa muhimu vilivyotakaswa hususani wakati huu wa COVID-19 ili kuwalinda watoto dhidi ya maambukizi. Mwaka huu wa 2020 umetangazwa na Umoja wa Mataifa kuwa mwaka wa wa wauguzi na wakunga ili kutambua mchango mkubwa wa wahudumu hawa wa sekta ya afya.
Hakuna aliye salama hadi kila mtu atakapokuwa salama dhidi ya COVID-19:UN
Juhudi kubwa na za kihistoria zinahitajika ili kuweza kulidhibiti janga la mlipuko wa corona au COVID-19 amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo alikuhutubia mkutano wa Muungano wa Ulya wa kutoa ahadi ya kupambana na janga hilo uliofanyika kwa njia ya mtandao mjini Brussels.
Mamilioni ya watoto hawataweza kusomea nyumbani-UNICEF
Taarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, iliyotolewa leo mjini Nairobi Kenya na Johannesburg Afrika Kusini, imeeleza kuwa zaidi ya watoto milioni 127 wa shule za awali, shule za msingi na sekondari Afrika Mashariki na Kusini, ambao walitakiwa kurejea shuleni wiki hii, wanasalia nyumbani kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19.