25 MACHI 2024
Hii leo jaridani mwenyeji wako ni Anold Kayanda akianzia na siku ya kimataifa ya kukumbuka watumishi wa UN wanaoshikiliwa vizuizini na wasiofahamika waliko, kisha anakwenda Sudan Kusini na harakati za kusaidia manusura wa ukatili wa kingono. Makala ni harakati za kumkomboa mwanamke na mashinani arejea Sudan Kusini.
22 MACHI 2024
Hii leo jaridani ikiwa ni Siku ya maji duniani, tunaangazia utunzaji wa vyanzo vya maji. Pia tunamulika mkutano wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW68 ambao umekunja jamvi hii leo. Makala tuankupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Tanzania kufuatilia jinsi ambayo miradi ya maji inavyoleta manufaa kwa jamii.
20 MACHI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya huduma za afya katika ukanda wa Gaza, na harakati za chanjo kwa watoto nchini Yemen. Makala tunasalia huko huko Gaza na mashinani inatupeleka nchini Tanzania kusikia ujumbe kuhusu siku ya furaha duniani.
18 MACHI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia baa la njaa unalowakumba waPalestina katika ukanda wa Gaza, na kesi zinazohusisha wanajeshi wa nchi ya Sudan Kusini. Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, na mashinani tunakupeleka nchini Kenya, kulikoni?