UNDP inahaha kuwasaidia waathirika wa matetemeko ya ardhi Afghanistan
Nchi ya Afghanistan hivi karibuni imekumbwa na matetemeko makubwa ya ardhi na kusababisha watu kupoteza maisha pamoja na uharibifu mkubwa. Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP linasema hadi kufikia Oktoba 14, zaidi ya watu 19,250 waliathirika na matetemeko katika jimbo la Herat.
Mazungumzo yanaendelea kupata ufafanuzi wa vikwazo na vizuizi kabla ya misaada kuingia Gaza
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliyeko nchini Misri leo ametembelea mpaka wa Rafah, kivuko pekee cha kuingia na kutoka Ukanda wa Gaza, ambako hivi sasa kuna mashambulizi yanaendelea kati ya Israel na wanamgambo wa kipalestina wa Hamas na kusema hivi sasa wanaendelea na mazungumzo kupata ufafanuzi wa vikwazo na vizuizi vya masharti yaliyowekwa na Israel kabla ya kuruhusu misaada ya kibinadamu kuingia Ukanda wa Gaza.