Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

14 Aprili 2022

Jaridani Aprili 14, 2022 na Leah Mushi

-Watu milioni 7 wameambukizwa chagas, upimaji na tib ani muhimu:WHO/UNITAID

-Tunazifuatilia taarifa kuwa Uingereza inataka kuwahamishia nchini Rwanda wasaka hifadhi

-Programu za mlo shuleni ni daraja la kufikia ndoto za elimu kwa watoto masikini :WFP

Sauti
11'34"

13 Aprili 2022

Jaridani na Leah Mushi kwanza ni habari kwa ufupi kisha katika mada kwa kina tunarejea makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa mahojiano maalum na waziri wa madini wa Tanzania kuhusu migogoro na rasilimali za madini ikiwemo almasi.

Mashinani ni athari za mgogoro wa Ukraine kwa uchumi wa nchi mbalimbai duniani.

Audio Duration
12'22"

12 Aprili 2022

Jaridani Jumanne, Aprili 12, 2022-

-Mashirika ya Umoja wa Mataifa yameonya kuwa janga lingine la njaa kama la mwaka 2011 linanyemelea Somalia iwapo wahisani hawataongeza ufadhili wao kwa ombi la usaidizi wa kibinadamu kwa taifa hilo la pembe ya Afrika kwa kuwa ukame wa muda mrefu sambamba na ongezeko la bei za vyakula vimeongeza idadi ya wasio na uhakika wa chakula kufikia watu milioni 6, sawa na asilimia 40 ya wananchi wote.

Sauti
14'13"

11 Aprili 2022

Jaridani Aprili 11, 2022 na Leah Mushi

Kwanza ni Habari kwa ufupi-

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP limetangaza programu ya kusaidia mahitaji ya mamilioni ya watu nchini Ukraine katika kipindi cha miaka miwili ijayo. 

8 Aprili 2022

Katika Jarida la Ijumaa Aprili 8, 2022 na Leah Mushi ameeanza na habari muhimu kwa siku ikiwemo:

Takriban watu milioni 15 wameathriwa vibaya na ukame nchini Kenya, Somalia na Ethiopia likwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM. 

Shirika hilo limeongeza kuwa huu ni ukame mbaya zaidi kuwahi kushuhudiwa katika miongo kadhaa ukisababisha mamilioni ya watu kutawanywa, kutokuwa na uhakia wa chakula na kuharibu ardhi ya kilimo na mazao.  

Sauti
12'57"

07 Aprili 2022

Ungana na Leah Mushi anayekuletea jarida hii leo likianza na maadhimisho ya siku ya afya, WHO imetoa wito kwa serikali na wananchi kwa ujumla kutunza mazingira. 

Leo pia ni siku ya kumbukizi ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda dhidi ya watutsi ya mwaka 1994 hayakuwa ya bahati mbaya ya yalikuwa yanaweza kuzuilika. 

pia utasikia kuhusu walinda amani wa Tanzania waliotembelea wafungwa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, Makala kutoka Zambia kuhusu ardhi oevu na ujumbe kwa watu kuendesha baiskeli kwa ajili ya kulinda afya zao. 

Karibu usikilize. 

Sauti
12'28"

5 Aprili 2022

Jaridani na Leah Mushi-

Watoto 3 kati ya 10 hawamalizi elimu ya msingi Madagascar : UNICEF

Nusu ya wananchi wote Afghanistan hawana uhakika wa chakula : FAO

Buriani walinda amani 8 wa Umoja wa Mataifa nchini DRC

Makala tunasalia DRC 

Mashinani ni wito kwa jamii ya kimataifa kuhusu kutokatisha msaada kwa Somali wakati hali ya utulivu ikiimarika.

Sauti
12'2"

4 Aprili 2022

Jaridani Aprili 4, 2022 na Leah Mushi 

-Karibu watu wote duniani, asilimia 99 wanavuta hewa isiyo salama iliyopita viwango vya ubora wa hewa vilivyowekwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na hivyo kutishia afya zao.

-Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antinio Guterres leo ameonya kwamba dunia inaelekea pabaya linapokuja suala la mabadiliko ya tabianchi ,na ni suala la aibu linaloambatana na ahadi hewa  zinazomuweka kila mtu kwenye hatari ya zahma kubwa.  

Sauti
11'28"

01 APRILI 2022

Kuelekea maadhimisho ya kuelimisha jamii kuhusu usonji tarehe 02 Aprili hii leo katika mada kwa kina tunakwenda nchini Kenya katika eneo la Roysambu jijini Nairobi, kwenye shule inayofundisha Watoto wenye usonji iitwayo, Kenya Community Center for Learning. 

Umoja Mataifa unataka ujumuishi wa Watoto wenye usonji ikiwa ni moja ya vipengele vya lengo namba 4 la malengo endelevu ya Umoja wa Mataifa, SDGs. Je nini kinafanyika huko, mwandishi wetu nchini Kenya, Thelma Mwadzaya ametuandalia mada hii kwa kina.

Sauti
11'22"