Nchini Sierra Leone mashine ya kukausha vitunguu yarejesha neema kwa wakulima
Vitunguu kuoza na kukosekana kwa kipato ulikuwa ni uhalisia kwa wakulima wa vitunguu kwenye mji wa Kabala nchini Sierra Leone wakati janga la COVID-19 lilipoibuka mapema mwaka 2020. Hali ilikuwa tete lakini kilio cha wakulima hao kilisikika na mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD ukaingilia kati.