Lazima tutokomeze ukeketaji : Mwanaharakati Ifra Ahmed
Kutana na mkimbizi kutoka Somalia, muathirika wa ukeketaji ambaye hakuacha athari za jinamizi hilo kusambaratisha ndoto zake za kuhakikisha hatopumzika hadi pale mangariba wote watakapobwaga manyanga na kuacha ukatili huo nchini Somalia na kwingineko duniani. Kulikoni Flora Nducha anasimulia zaidi
(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)
Jina langu ni Ifrah Ahmed
Dublin nchini Ireland maskani ya kudumu ya Ifra mkimbizi wa zamani aliyegeuka kuwa mwanaharakati wa kupinga ukeketaji na sasa anajivunia kuwa raia wa taifa hilo la barani Ulaya.